KITABU CHA KILELE CHA UBEPARI NA TISHIO LA USHOGA. (SEHEMU YA KWANZA)


YALIYOMO



SHUKRANI
Shukrani za dhati kwa Mungu baba aliye juu kwa kunipa uhai na kuniwezesha kufanikisha kutoka kwa kitabu hiki ingawa ilikuwa kazi ngumu bila msaada wako Mungu nisingeweza kufanikisha hili.
Pia shukrani zangu ziwafikie familia yangu na marafiki zangu kwa kunipa ushirikiano wa kutosha Mungu awabariki nyote.
Bila kukusahau wewe uliyechukuwa muda wako kosa kitabu hiki Mungu akubariki sana na kukutia nguvu katika maangaiko yako ya kila siku.PAMOJA TUNAWEZA.


KILELE CHA UBEPARI  NA TISHIO LA USHOGA AFRIKA
Kitabu hiki kinaelezea maisha halisi ya mwananchi wa hali ya chini katika bara la Afrika,ususani chini ya ya jangwa la sahara.
Harakati zao za kujinasua katika umasikini uliokisiri?
Ni  kwa nini umasikini unazidi kuongezeka ndani ya bara letu lenye kila aina ya rasilimali?.Je ni kwa nini wanasiasa wamekuwa vigeugeu?.
Nani anayeanzisha maandamano ya ukombozi katika nchi nyingi za Africa?
·         lengo la kuleta ushoga Africa nini?
·         ni nani wa kulaumiwa katika  hili?
Kitabu hichi kimechambua kwa undani nini cha kufanya ili kujikomboa katika hili janga lilokumba bara letu la africa.
hapa tulipo sasa ni KILELE CHA UBEPARI KATIKA BARA LETU.(KILELE CHA UBINAFSI WA MALI)














 UTANGULIZI

Tujikumbushe kwanza Africa ilitoka wapi ?Africa kama mabara mengine dunia  lilikuwa bara lenye wananchi wanaojiongoza kwa  mila na desturi za makabila yao.Hii ikimaanisha kuwa sheria na taaratibu za kuishi zilizingatia sana mila na desturi hiyo basi kila ukoo ulifanya kila mbinu ili uweze kukubalika katika kabila husika na waweze kupewa uongozi wa kabila husika,hali hii ilifanya kupatikana kwa ukoo zenye nguvu ya kutawala na kutoa maamuzi mazito kuhusu makabila husika.
 Katika hali hii iliongeza ubunifu hasa katika maeneo ya uzalishaji wa mazao na vifaa vya kivita na mafunzo ya kijeshi.hii ilisaidia sana ukuwaji wa maeneo na kusababisha koo na makabila mengine madogo madogo kufa kwa sababu ya kushindwa  kivita na mali zao walizokuwa wakimiliki kupokonywa na makabila hayo yakageuka vibaraka wa makabila yale makubwa.
Makabila mengi yalipotea nakutofahamika tena kwenye uso wa dunia kutokana na sababu hizo na mengine yaliweka makazi kwenye maeneo yenye wanyama wakali ,mafuriko na wadudu waambukizao maradhi  na wakashambuliwa na magonjwa,wanyama wakali na mafuriko  na kuisha taratibu baada ya kuanza kutawanyika kukimbia majanga hayo.



Je ubepari ulianzia wapi?
Tutambue kuwa ubepari huanza kwa hatua hiyo basi historia inaonyesha kuwa toka aumbwe Adamu na Eva hapo ndipo ubepari ulipoaza ukiwa na sura ya ubinafsi(maana ubinafsi ni mtoto wa ubepari).Adamu na Eva walipewa dunia waitawale na wafaidi kila kitu kilichopo ndani ya dunia hii mto,maziwa ,asali ,matunda, majani na kadhalika.
Adamu na Eva alijua kabisa bosi wao ni Mungu aliye juu mmiliki wa mali zote walizokabiziwa wazitumie mpaka pumzi yao pia ilikuwa ni mali yake.
Adamu na Eva  walingizwa kishawishini na shetani wamsaliti Mungu na kubinafsisha mali zake zote walizokabiziwa na wazimiliki wao kwa ushirikiano na shetani mkuu wa kuzinu.
Kutokana na hilo bwana Mungu alichukiza na ile hali na kuamua kuwatupa nje ya ile bustani ya edeni na kuwaacha wakahajitafutie wenyewe chakula na mahitaji yao ya kila siku.
Katika hali hii basi tutaona kuwa mwenyekiti wa ubepari duniani ni SHETANI.
Maana ndiye muanzilishi waubepari duniani toka enzi za Adamu na Eva ni yeye aliyewapa ujasiri wakina Adamu na Eva waukubali ubinafsi na kuachana na mpango wa Mungu ulikuwa unaweka umoja wa kila kitu.


Je dhumuni la ubepari ni nini?
Katika hali ya kawaida tunaona kuwa dhumuni kubwa la ubepari dunia ni uuwaji,nikimaanisha kuwa shetani alikuwa anaamini kuwa pindi adamu na eva watapomsaliti mungu basi mungu atawaacha wapweke na kwa sababu ya mateso na masumbuko ya dunia watu hawa watashindwa kusitahimili mateso hayo na kufa na kuacha mali zote chini ya hima yake muovu shetani.
Imani ya shetani ilikuwa kuu akiamini kuwa hata kama wataweza kuzaa na kuongezeka basi kizazi watachokizaa watakirisisha dhambi kuu ya ubinafsi ambayo ni kitovu cha ubepari na mwisho wa nyakati watauana wenyewe kwa wenyewe wakigombania malisho na chakula.
Eneo la wazi

Safari za wafanyabiashara ziliwezesha kugundulika kwa bara hili  la kwa mataifa ya magharibi na asia kwa ujumla wake.Bara letu lilionekana kuwa eno la wazi lisilo na miliki wenye nguvu kwa kuwa kulikuwa na makabila waliokuwa wamejitenga sana kiumbali na huku yakijishuhulisha nza shuhuli mbalimbali ikiwemo uvuvi,ufugaji na mengine kilimo basi nchi za bara la ulaya waliamua kwa dhati kushambulia bara hili kila kona na kujichumia mali zilizopo na pia walichukuwa watu wa bara hili na kwenda kuwafanyisha kazi ngumu kwenye mashamba na viwandani. Hakuna kilichokuwa si mali kwao, vyote walibeba si pembe za ndovu,watu ,madini wala bidhaa za utamaduni.Ingawa maeneo mengine walipata vizuizi  kutoka kwa makabila kadhaa yaliokuwa na vifaa vya kivita na kundi kubwa la wapiganaji lakini kwao haikuwa shida kubwa maana walikuwa wamesha jipanga sawa sawa kuvunja kizuizi chochote kile kitachokuwa kinajitokeza na kuzuia mpango yao.huku wakitengeneza ramani ya kuonyesha sehemu zenye mali ikiwemo madini na maeneo yanayofaa kwa kilimo walifanya kazii hii kwa uangalifu mkubwa.

SOMA KITABU HIKI CHOTE HAPA SASA 

No comments:

Post a Comment